Friday, April 17, 2015

WAKILI WA GWAJIMA AMEANDIKA HAYA BAADA YA KUTOKA MAHAKAMANI KISUTU LEO MCHANA AKIWA NA MTEJA WAKE ASKOFU GWAJIMA

Tumetoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Dar es Salaam iliyopo
Kisutu ambapo Askofu Josephat Gwajima ameshtakiwa kwa;
(1).Kutoa lugha ya matusi kwa Polycarp Cardinal Pengo.
Mahakama imemuachia Askofu Gwajima kwa dhamana ya
kujidhamini yeye mwenyewe.(2). Kufanya uzembe katika silaha
anayomiliki kisheria kiasi kwamba ikaangukia mikononi kwa
Askofu Yeconia Bihagaze na wenzake wawili, na kwa Askofu
Bihagaze na wenzake wawili kupatikana na silaha na risasi
wakati siyo wamiliki halali wa Silaha hiyo inayomilikwa na
Askofu Gwajima. Mahakama imewaachia washtakiwa wote kwa
kudhaminiwa na mdhamini mmoja mmoja.
Case itatajwa tarehe 4 April.
Mpaka tunakwenda Mahakamani Jeshi la Polisi halijajibu Barua
yetu ya kutaka watutajie kifungu cha Sheria kinachowapa
mamlaka ya kudai nyaraka zinazohusiana na umiliki wa
helicopter na usajili wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania
Church/Ufufuo na Uzima na nyinginezo, na wala Askofu
Gwajima na wenzake hawajashtakiwa kwa chochote kuhusiana
na suala hilo.

No comments:

Post a Comment