Saturday, May 2, 2015

FLOYD MAYWEATHER AMDUNDA PACQUIAO

Floyd Mayweather amemdunda Manny Pacquiao kwa
points baada ya pambano la dunia lililokuwa
likisubiriwa kwa hamu kumalizika huko jijini Las
Vegas.
Pacquiao kama ilivyokuwa ikitarajiwa alirusha ngumi
nyingi zaidi kuliko mpinzani wake lakini Mayweather
aliweza kurusha ngumu zenye faida zaidi
zilizowafanya majaji wanne wampe ushindi.
Mayweather ameshinda kwa point 118-110, 116-112,
116-112. Kwa ushindi huo, Mayweather ameendelea
kushikiliza rekodi yake ya kutowahi kushindwa katika
mapambano yake 48 aliyowahi kupigana.
Tazama picha za pambano hilo.



No comments:

Post a Comment