Wednesday, May 20, 2015
MAPAMBANO YATOKEA MKOANI NJOMBE KATI YA POLISI NA RAIA
Monday, May 4, 2015
WAZIRI MKUU AUNDA KAMATI KUSHUGHULIKIA USAFIRI
WAZIRI MKUU AUNDA KAMATI KUSHUGHULIKIA
USAFIRI
Waziri Mkuu , Mizengo Peter Pinda ameunda kamati maalumu ya
kudumu ya kusimamia Usafiri wa barabarani nchini ili kutatua
changamoto zinazoikabali sekta ya Usafiri .
Katika kamati hiyo mwenyekiti wake atakuwa katibu mkuu wa
wizara ya chukuzi, Katibu akiwa kamishna wa polisi barabarani
na Mkurugenzi wa SUMATRA huku wajumbe wakiwa ni pamoja
na katibu mkuu wizara ya kazi ya na ajira , katibu mkuu ujenzi,
mwanasheria mkuu wa serikali na naibu katibu mkuu ofisi ya
waziri mkuu .
Mkuu wa ratibu wa idara ya maafa toka ofisi ya waziri mkuu ,
mwenyekiti wa TABOA na TATOA , CHAKUA na wanatakiwa
kuanza kufanya vikao leo na kila mwezi watakutana kujadili na
kutatua changamoto zote kasoro zile za kisheria ambazo
zitapelekwa serikalini kwa mchakato zaidi wa kuzirekebisha.
Wakati huo huo umoja wa vyama vya madereva nchini Tanzania
umesema hauna taarifa juu ya wao kutakiwa kukutana na waziri
mkuu Mh . Mizengo Pinda kwa ajili ya mazungumzo kama
inavyozungumzwa na kusisitiza kuwa wao wataendelea na
mgomo wao ulioanza leo mpaka masuala yao yatapofanyiwa
kazi .
Akizungumza na East Africa Radio leo Makamu Mwenyekiti wa
Muungano wa vyama vya Madereva Abdallah Lubala amesema
kauli ya kuwa wamekubaliana kukutana na Mh. Pinda ni za
kisiasa na hazina ukweli wowote hivyo wataendelea na mgomo
wao.
Wakati huo huo mgomo huo ambao umetangazwa kwa nchi
nzima athari zake zimejitokeza katika mikoa mingine tofauti
ambapo madereva wa mabasi ya abiria wamegoma huku
wasafiri wakitumia usafiri mbadala wa bajaji pamoja bodaboda .
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi wa jiji la
Mbeya , Arusha na Mwanza wamesema kuwa wanalazimika
kutembea umbali mrefu kwenda makazini na wangine wakitumia
gharama kubwa kutokana na vyombo hivyo wanavyotumia
kupandisha bei za nauli kuliko kawaida .
( CHANZO : EAST AFRICA RADIO )
Saturday, May 2, 2015
FLOYD MAYWEATHER AMDUNDA PACQUIAO
Floyd Mayweather amemdunda Manny Pacquiao kwa
points baada ya pambano la dunia lililokuwa
likisubiriwa kwa hamu kumalizika huko jijini Las
Vegas.
Pacquiao kama ilivyokuwa ikitarajiwa alirusha ngumi
nyingi zaidi kuliko mpinzani wake lakini Mayweather
aliweza kurusha ngumu zenye faida zaidi
zilizowafanya majaji wanne wampe ushindi.
Mayweather ameshinda kwa point 118-110, 116-112,
116-112. Kwa ushindi huo, Mayweather ameendelea
kushikiliza rekodi yake ya kutowahi kushindwa katika
mapambano yake 48 aliyowahi kupigana.
Tazama picha za pambano hilo.