Mapigano makali yanaendelea sasa mjini Njombe kati ya wananchi
na polisi tangu asubuhi.
Mtangazaji wa Kings FM ya Njombe, King David, ametutumia taarifa
ifuatayo:
Jana usiku wa saa 3 polisi wa doria walikua mtaani wakapita mtaa
mmoja unaitwa Nzenge kuna kilabu cha pombe za kienyeji
wakawakuta watu mle ndani. Sasa katika kuwauliza kwanini wapo
eneo hilo mpaka muda wa usiku, wananchi wakajibu kuwa muda wa
kufunga ni saa 4 na ndio utaratibu ofcoz (Kufunga saa 4) wale polisi
hawakuridhishwa na majibu na kuamua kuwatimua wananchi pale
ndani lakini jamaa hawakutii. Polisi wakafyatua risasi ambayo
ilimpata mwananchi mmoja na kumuua pale pale huku mmoja
akijeruhiwa.
Then polisi wakaondoka baada ya tukio hilo bila msaada wowote.
Wananchi wakapanic na ilipofika asubuhi leo wananchi wa mtaa ule
pamoja na vijana wa boda boda wakaanza maandamano kwenda
kituo cha polisi cha mkoa wakiwa wanatamka maneno makali sana
ikiwa ni pamoja na kuwataka polisi wachukue mwili wa marehemu
na kuuzika wao pamoja na kutoa sababu za kufanya mauaji hayo.
Polisi wakaanza kuwatimua tena lakini wananchi wakagoma ndo
hapo polisi walipoamua kutumia nguvu ya ziada ikiwa ni pamoja na
kupiga mabomu ya machozi na risasi hewani. Bado wananchi
walikua wagumu kuelewa mpaka walipoamua kuanza kuwapigwa
kwa virungu, fimbo na mateke.
Polisi wametoa tahadhari ya watu kutotoka nje na kuna dereva
mmoja amepigwa risasi tena mchana huu kauawa pia kuna baadhi
ya polisi wamejeruhiwa kwa mawe na mapanga kutoka kwa
wananchi.
Kwasasa hakuna mtu anaruhusiwa kutoka nje.
No comments:
Post a Comment