Saturday, October 3, 2015

MCHUNGAJI MTIKILA APATA AJALI NA KUFARIKI

Wakuu, 

Kuna taarifa kwamba Mchungaji Christopher Mtikila amepata ajali ya gari mkoani Pwani alfajiri ya leo, taarifa zaidi tunasubiria kutoka kwa Kamanda wa Polisi mkoani humo.

=====
UPDATE:

JamiiForums imeongea na Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Jafari Mohamed, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa "Taarifa za mwanzo" zinasema amefariki saa 12 kasorobo asubuhi katika kijiji cha Msolwa, Chalinze.

Amesema gari lililokuwa limempakia lilikuwa linatokea Morogoro na kwamba walikuwa watu wanne ambapo wengine watatu wamejeruhiwa vibaya.

Majeruhi wamekimbizwa katika Hospitali ya Tumbi.

Saturday, July 18, 2015

MAJINA YA WASHINDI WA MTV ManaSsas 2015

MAJINA Ya Washindi wa MTV Mama Awards 2015 ‪#‎MTVMAMA2015‬


List ya Washindi wote hii hapa..

Best Female:

Yemi Alade (Nigeria) >>> Mshindi.

Bucie (South Africa)

Busiswa (South Africa)

Seyi Shay (Nigeria)

Vanessa Mdee (Tanzania)

Best Male:

Davido (Nigeria) >>> Mshindi

AKA (South Africa)

Diamond (Tanzania)

Sarkodie (Ghana)

Wizkid (Nigeria)

Best Group:

P Square (Nigeria) >>> Washindi.

B4 (Angola)

Beatenberg (South Africa)

Black Motion (South Africa)

Sauti Sol (Kenya)

Best New Act Transformed by Absolut:

Patoranking (Nigeria) >>> Mshindi.

Anna Joyce (Angola)

Cassper Nyovest (South Africa)

Duncan (South Africa)

Stonebwoy (Ghana)

Best Hip Hop: 

Cassper Nyovest (South Africa) >>>Mshindi.

K.O. (South Africa)

Phyno (Nigeria)

Olamide (Nigeria)

Youssoupha (DRC)

Best Collaboration:

AKABurna BoyDa LES & JR: “All 

Tuesday, June 30, 2015

Watch Ali kiba _chekecha official video

Watch "Alikiba - Chekecha Cheketua (Official Video)" on YouTube - https://youtu.be/ZbCmbWktYh4

Sunday, June 14, 2015

AJALI MBAYA YATOKEA IRINGA



Basi la abiria la Another G limepata ajali eneo la Kinyanambo Mafinga wilaya ya Mufindi katika mkoa wa Iringa. Gari hilo limegongana usokwa uso na lori aina ya Scania ambapo taarifa za awali zinaeleza kwamba kutoka kwenye gari hilo la abiria wamefariki watu 23 wakati kutoka kwenye lori amepona mtu mmoja pekee na wengine wote wamefariki akiwemo dereva wa lori hilo.

Aidha wakazi wa maeneo jirani ambapo ajali hiyo imetokea wameeleza kwamba ajali hiyo ni mbaya sana.

Ndugu msomaji wa mtandao huu endelea kufuatilia mtandao huu kwa habari zaidi juu ya ajali hii.

Saturday, June 13, 2015

WASHINDI WA TUZO ZA KILIMANJARO MUSIC AWARDS 2015

ENTERTAINMENT

Orodha kamili ya washindi wa Kilimanjaro Music Awards 2015.

Hii ni orodha kamili ya washindi wa tuzo za muziki Tanzania Kilimanjaro Music Awards 2015 zilizofanyika 13 June 2015 Mlinani City jijini Dar es salaam.

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mtumbuizaji Bora wa Muziki wa Kiume wa Mwaka ameshinda>Ali Kiba.

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mwimbaji bora wa kike Bongo Fleva ameshinda> Vanessa Mdee aka V Money

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Msanii Bora wa Kiume Taarab ameshinda >Mzee Yusuph

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mwimbaji Bora wa Kike Taarab ameshinda> Isha Mashauzi.

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mwimbaji Bora wa Kiume Kutoka Bendi ameshinda >Jose Mara

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Wimbo Bora wa Mwaka wa Muziki wa Taarab imeshinda >Mapenzi Hayana Dhamana Yake Isha Mashauzi

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Wimbo Bora wa Mwaka imeshinda ‘Mwana‘ Ya Ali Kiba

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Wimbo Bora wa Kiswahili Kutoka Bendi imeshinda >’ Walewale ‘ ya FM Academia

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Wimbo Bora wa Muziki wa R&B imeshinda single ya Jux >‘Sisikii’

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Wimbo Bora wa Hip Hop imeshinda single ya Profesa Jay> Kipi Sijasikia Ft Diamond @diamondplatnumz

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Wimbo Bora wa Reggae&Dance Hall ameshinda > Maua Sama

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Rapa Bora wa Mwaka Muziki wa Bendi ameshinda> Ferguson

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Msanii Bora wa Hip Hop Ameshinda >Joh Makini

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Wimbo Bora wa Afrika Mashariki wameshinda Kenya >Sauti Sol Kupitia wimbo wao wa Sura Yako

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mtunzi Bora wa Mwaka Taarab ameshinda >Mzee Yusuph
go
#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mtunzi Bora wa Mwaka Muziki wa Bongo Fleva ameshinda> Ali Kiba.

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mtunzi Bora wa Mwaka muziki wa Bendi ameshinda > Jose Mara

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Msanii Bora Chipukizi ameshinda >Baraka Da Prince

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mtunzi Bora wa Mwaka Hip Hop imeshindwa na >Joh Makini

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Bendi Bora ya Mwaka wameshinda> FM Academia

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mtayarishaji Bora wa Nyimbo wa Mwaka Muziki wa Bongo Fleva ameshinda > Nahreel

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mtayarishaji Bora wa Nyimbo wa Mwaka Taarab ameshinda> Enrico

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Mtayarishaji Bora wa Nyimbo wa Mwaka Bendi ameshinda> Amoroso

#FahamuKTMA2015 Tuzo ya Wimbo Bora Wenye Vionjo vya Asili ya Kitanzania ameshinda> Mrisho Mpoto

#FahamuKTMA2015 Kikundi Bora cha Mwaka Muziki wa Taarab wameshinda  >Jahazi Modern Taarab

#FahamuKTMA2015 Kikundi Bora cha Mwaka Muziki Wa Bongo Fleva Wameshinda >Yamoto Band

Friday, June 5, 2015

SAMWEL SITTA ACHUKUA FOMU, ATAKA MIAKA 5 TU KUWANG'OA WATU HAWA




Waziri wa Uchukuzi Samweli Sitta akionesha fomu ya kugombea urais mara katika ukumbi wa NEC makao makauu Dodoma.

  

Waziri wa Uchukuzi Mh. Samweli Sitta akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kuchukua fomu leo.

Waziri wa Uchukuzi  Mh. Samweli Sitta leo  amechukua fomu ya kugombea urais kwa tiketi ya  chama cha Mapinduzi makao makuu ya CCM yaliyopo White House  Dodoma  mjini. Sitta ameambatana na Mke wake pamoja na wapambe wake.

Akizungumza mara baada ya kupokea fomu Sitta amesema kwamba  anaomba   miaka mitano tu sio zaidi ili aweze kuwashughulikia ipasavyo mafisadi na kumaliza kabisa tatizo la ufisadi  unao onekana kukwamisha maendeleo ya ya  nchi Hivisasa.

Aidha, ametaja vipaumbele vyake kuwa ni;

(i) Kuulinda muungano
(ii)  Kumalizia mchakato wa katiba Pendekezwa
(iii)  Kumaliza kabisa suala la Rushwa
(iv) Kuleta mahusiano mazuri kati ya  Wafanyabiashara na Serikali
(v) Kuimarisha Chama 

Wednesday, May 20, 2015

MAPAMBANO YATOKEA MKOANI NJOMBE KATI YA POLISI NA RAIA

Mapigano makali yanaendelea sasa mjini Njombe kati ya wananchi
na polisi tangu asubuhi.
Mtangazaji wa Kings FM ya Njombe, King David, ametutumia taarifa
ifuatayo:
Jana usiku wa saa 3 polisi wa doria walikua mtaani wakapita mtaa
mmoja unaitwa Nzenge kuna kilabu cha pombe za kienyeji
wakawakuta watu mle ndani. Sasa katika kuwauliza kwanini wapo
eneo hilo mpaka muda wa usiku, wananchi wakajibu kuwa muda wa
kufunga ni saa 4 na ndio utaratibu ofcoz (Kufunga saa 4) wale polisi
hawakuridhishwa na majibu na kuamua kuwatimua wananchi pale
ndani lakini jamaa hawakutii. Polisi wakafyatua risasi ambayo
ilimpata mwananchi mmoja na kumuua pale pale huku mmoja
akijeruhiwa.
Then polisi wakaondoka baada ya tukio hilo bila msaada wowote.
Wananchi wakapanic na ilipofika asubuhi leo wananchi wa mtaa ule
pamoja na vijana wa boda boda wakaanza maandamano kwenda
kituo cha polisi cha mkoa wakiwa wanatamka maneno makali sana
ikiwa ni pamoja na kuwataka polisi wachukue mwili wa marehemu
na kuuzika wao pamoja na kutoa sababu za kufanya mauaji hayo.
Polisi wakaanza kuwatimua tena lakini wananchi wakagoma ndo
hapo polisi walipoamua kutumia nguvu ya ziada ikiwa ni pamoja na
kupiga mabomu ya machozi na risasi hewani. Bado wananchi
walikua wagumu kuelewa mpaka walipoamua kuanza kuwapigwa
kwa virungu, fimbo na mateke.
Polisi wametoa tahadhari ya watu kutotoka nje na kuna dereva
mmoja amepigwa risasi tena mchana huu kauawa pia kuna baadhi
ya polisi wamejeruhiwa kwa mawe na mapanga kutoka kwa
wananchi.
Kwasasa hakuna mtu anaruhusiwa kutoka nje.

Monday, May 4, 2015

WAZIRI MKUU AUNDA KAMATI KUSHUGHULIKIA USAFIRI

WAZIRI MKUU AUNDA KAMATI KUSHUGHULIKIA
USAFIRI

Waziri Mkuu , Mizengo Peter Pinda ameunda kamati maalumu ya
kudumu ya kusimamia Usafiri wa barabarani nchini ili kutatua
changamoto zinazoikabali sekta ya Usafiri .
Katika kamati hiyo mwenyekiti wake atakuwa katibu mkuu wa
wizara ya chukuzi, Katibu akiwa kamishna wa polisi barabarani
na Mkurugenzi wa SUMATRA huku wajumbe wakiwa ni pamoja
na katibu mkuu wizara ya kazi ya na ajira , katibu mkuu ujenzi,
mwanasheria mkuu wa serikali na naibu katibu mkuu ofisi ya
waziri mkuu .
Mkuu wa ratibu wa idara ya maafa toka ofisi ya waziri mkuu ,
mwenyekiti wa TABOA na TATOA , CHAKUA na wanatakiwa
kuanza kufanya vikao leo na kila mwezi watakutana kujadili na
kutatua changamoto zote kasoro zile za kisheria ambazo
zitapelekwa serikalini kwa mchakato zaidi wa kuzirekebisha.
Wakati huo huo umoja wa vyama vya madereva nchini Tanzania
umesema hauna taarifa juu ya wao kutakiwa kukutana na waziri
mkuu Mh . Mizengo Pinda kwa ajili ya mazungumzo kama
inavyozungumzwa na kusisitiza kuwa wao wataendelea na
mgomo wao ulioanza leo mpaka masuala yao yatapofanyiwa
kazi .
Akizungumza na East Africa Radio leo Makamu Mwenyekiti wa
Muungano wa vyama vya Madereva Abdallah Lubala amesema
kauli ya kuwa wamekubaliana kukutana na Mh. Pinda ni za
kisiasa na hazina ukweli wowote hivyo wataendelea na mgomo
wao.
Wakati huo huo mgomo huo ambao umetangazwa kwa nchi
nzima athari zake zimejitokeza katika mikoa mingine tofauti
ambapo madereva wa mabasi ya abiria wamegoma huku
wasafiri wakitumia usafiri mbadala wa bajaji pamoja bodaboda .
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi wa jiji la
Mbeya , Arusha na Mwanza wamesema kuwa wanalazimika
kutembea umbali mrefu kwenda makazini na wangine wakitumia
gharama kubwa kutokana na vyombo hivyo wanavyotumia
kupandisha bei za nauli kuliko kawaida .
( CHANZO : EAST AFRICA RADIO )

Saturday, May 2, 2015

FLOYD MAYWEATHER AMDUNDA PACQUIAO

Floyd Mayweather amemdunda Manny Pacquiao kwa
points baada ya pambano la dunia lililokuwa
likisubiriwa kwa hamu kumalizika huko jijini Las
Vegas.
Pacquiao kama ilivyokuwa ikitarajiwa alirusha ngumi
nyingi zaidi kuliko mpinzani wake lakini Mayweather
aliweza kurusha ngumu zenye faida zaidi
zilizowafanya majaji wanne wampe ushindi.
Mayweather ameshinda kwa point 118-110, 116-112,
116-112. Kwa ushindi huo, Mayweather ameendelea
kushikiliza rekodi yake ya kutowahi kushindwa katika
mapambano yake 48 aliyowahi kupigana.
Tazama picha za pambano hilo.



Friday, April 17, 2015

WAKILI WA GWAJIMA AMEANDIKA HAYA BAADA YA KUTOKA MAHAKAMANI KISUTU LEO MCHANA AKIWA NA MTEJA WAKE ASKOFU GWAJIMA

Tumetoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Dar es Salaam iliyopo
Kisutu ambapo Askofu Josephat Gwajima ameshtakiwa kwa;
(1).Kutoa lugha ya matusi kwa Polycarp Cardinal Pengo.
Mahakama imemuachia Askofu Gwajima kwa dhamana ya
kujidhamini yeye mwenyewe.(2). Kufanya uzembe katika silaha
anayomiliki kisheria kiasi kwamba ikaangukia mikononi kwa
Askofu Yeconia Bihagaze na wenzake wawili, na kwa Askofu
Bihagaze na wenzake wawili kupatikana na silaha na risasi
wakati siyo wamiliki halali wa Silaha hiyo inayomilikwa na
Askofu Gwajima. Mahakama imewaachia washtakiwa wote kwa
kudhaminiwa na mdhamini mmoja mmoja.
Case itatajwa tarehe 4 April.
Mpaka tunakwenda Mahakamani Jeshi la Polisi halijajibu Barua
yetu ya kutaka watutajie kifungu cha Sheria kinachowapa
mamlaka ya kudai nyaraka zinazohusiana na umiliki wa
helicopter na usajili wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania
Church/Ufufuo na Uzima na nyinginezo, na wala Askofu
Gwajima na wenzake hawajashtakiwa kwa chochote kuhusiana
na suala hilo.

Thursday, April 9, 2015

KESI YA MINJA YAPIGWA CALENDAR TENA


THURSDAY , 9TH APR , 2015

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini, Johnson Minja leo amefikishwa mahakamani kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali ya kesi inayomkabili ya uchochezi, lakini upande wa serikali ulikuwa haujakamilisha kuandika maelezo hayo.

Mwendesha mashtaka mwandamizi wa serikali, Rose Shio aliiambia mahakama kuwa kesi hiyo ilifika mahakamani hapo leo kwa ajili ya kusikilizwaji wa awali lakini upande wa serikali ulikuwa bado haujakamilisha kuandika maelezo hayo ya awali.

Mweyekiti wa Shirikisho la vyama vya Wafanyabiashara nchini, Bw. Jonson Minja (aliyevaa koti jeusi) huku akiongea na katibu wake Mchungaji Kiondo


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini, Johnson Minja leo amefikishwa mahakamani kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali ya kesi inayomkabili ya uchochezi, lakini upande wa serikali ulikuwa haujakamilisha kuandika maelezo hayo.

Mwendesha mashtaka mwandamizi wa serikali, Rose Shio aliiambia mahakama kuwa kesi hiyo ilifika mahakamani hapo leo kwa ajili ya kusikilizwaji wa awali lakini upande wa serikali ulikuwa bado haujakamilisha kuandika maelezo hayo ya awali.

Amesema kuwa kesi hiyo leo imekuja mahakamani kwa ajili ya usikilizwaji wa awali lakini kwa bahati mbaya upande wa serikali umeshindwa kuandika maelezo ya awali kwa hiyo akaomba ipangwe tarehe nyingine kwa ajili ya kusikiliza maelezo ya awali ya kesi hiyo.

Wakili wa mshtakiwa huyo Godfrey Wasonga amesema hana kipingamizi na ombi hilo la mwendesha mashtaka wa serikali na kuomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya usikilizwaji wa awali.

Baada ya maelezo hayo, hakimu mfawidhi wa mahakama ya Wilaya ya Dodoma, Rhoda Ngimilanga alisema kesi hiyo itatajwa tena Mei 7 mwaka huu na mshtakiwa ameendelea kuwa nje kwa dhamana.

Sunday, January 4, 2015

FIDEL ODINGA MTOTO WA RAILA ODINGA AKUTWA AMEFARIKI DUNIA

Fidel Odinga Mtoto Mkubwa wa kiume wa
Mwanasiasa maarufu nchini kenya Raila
Odinga amekutwa amefariki ndani ya chumba
chake alimokuwa amelala leo alfajiri, Police
nchini kenya muda huu wanaendelea na
uchunguzi mkali kubaini chanzo kama
kinahusiana na mambo ya siasa, Hivi
karibuni Raila Odinga amekuwa akiibana na
kuishurtumu Serikali ya Kenyata kwa
kushindwa kuwalinda wakenya hasa
kutokana na mauaji ya Al shabab, Pia
Wapinzani kupinga muswada ambao tayari ni
sheria ya Ugaidi nchini kenya ambao Raila
anaona hauwalindi wakenya.
From Kenya-Today blog:
Fidel died at Nairobi Hospital where he was
rushed by his wife last night. It is not yet
known what killed hill.
Fidel had lunch with his dad on Sunday at
Raila’s his Karen home. Raila told The Star
this morning he was fine.
He then went out in the evening with some
friends and came home at around 1am, he is
said to have had breathing problems and
was rushed in an ambulance to Nairobi
Hospital where he died.
Raila confirmed the death of his son, he is at
the scene