Thursday, October 30, 2014

WOLPER AONGEA KWA UCHUNGU KUPITIA HILI GAZETI NA KUKANUSHA HII HABARI

NAOMBA MNISHAURI KUHUSU HILI GAZETI MKIWA KMA MASHABKI ZANGU MAANA AKUNA UKWELI ...NA JE NIVEMA KWEL MAANA TUNAWAZAZI NA PIA TUNA WAPENZI SASA MTU UTAANZA KUJIELEZEA VP KWA MPENZ WAKO ILI AKUELEWE KWAMBA HZI HABAR SYO ZAKWELI...LAKN PIA ALLY KBA NINGEPENDA UANDIKE CHOCHOTE KMA NI KWENYE ACC YAKO AU UTAJBU HAPA KWANGU ..HII NI KWA UPANDE WANGU...HOPE IREN PIA KMA KAGUSWA NAE ATAANDIKA UKWEL WAKE..NIPO MWANZA KIKAZI GAZET HILI LIMENIKOSESHA RAHA SAANA ...NAOMBENI USHAUR WENU NAMSAADA PIA ATA KMA NIKESI NPO TAYAR ASANTENI KWAKUPOTEZA MUDA WENU..LKN PIA ANAEJUA KUNA MTU MTETEZ AU ANAIJUA SHERIA UMTAG..AMEN

BREAKING:MSANII MANENTO AFARIKI DUNIA

Habari zilizotufukia hivi punde zinasema kuwa muigizaji Mzee Manento amefariki dunia hapo jana. Bado tunafuatilia kwa karibu habari hizi nz chanzo ch kifo cha mzee wetu huyu.

Mzee Mnento atakumbukwa hasa kwa filamu alizocheza kiumakin na marehemu Kanumba. Hero of the church, Dar to lagos,fake pastor n.k pumzika kwa Amani

Mungu ailaze Roho ya maerehemu mahali pema peponi amina. 

Wednesday, October 29, 2014

MSANII NAY WA MITEGO NA MPENZI WAKE WAPATA MTOTO

Mchumba wa rapper Nay wa Mitego, Siwema amejifungua mtoto wa kiume jana ambapo pia ilikuwa ni siku ya kuzaliwa kwa mama wa msanii huyo.
Mtoto wa Nay akiwa na bibi yake

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nay ameandika:Ooooooh my goooooood!!!! Leo ni cku ya kuzaliwa mama angu mzazi,,, tukiwa 2nakata cake napigiwa cm nimepata mtoto wakiume… yani kazaliwa cku 1 na bibi yake,,! Hao apo wamezaliwa leo… Asante Mungu.. Asante

DIAMOND KUTUNUKIWA PHD

DIAMOND KUTUNUKIWA PHD.!
Tarifa kutoka Idara ya Sanaa ya Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)
zinasema kuwa tarehe 8 Novemba 2014,
Kijana Nassib Abdul atatunukiwa Shahada
ya Uzamivu(Phd) na Chuo hicho kwa
kuthamini mchango wake kwenye jamii
kupitia sanaa.(Honorary PhD in Fine
&Perfoming Arts).
Alongside DIAMOND mwingine
atakayepewa Shahada hii ya Heshima
kwenye Mahafali haya ni Balozi Fulgence
Kazaura (marehemu) ambaye aliwahi kuwa
Chancellor wa UDSM miaka ya nyuma!!
Naibu Mkuu wa shule ya Sanaa na
Sayansi ya Jamii (College of Arts and
Social Sciences) Prof.H Sigala amekiri
kupokea maombi kutoka Idara ya Sanaa
za Maonesho (Department of Fine
&Perfoming Arts) ya kumtunuku Diamond
PhD.
Amesema bado haijadhibitika kama
Diamond atatunukiwa shahada hiyo hadi
bodi ya taaluma ya chuo (senate) ikae na
kupitia maombi hayo. “Senate ikikaa
inaweza kukubali au kukataa maombi
hayo, lakini kwa sasa hatuwezi kusema
lolote” alisema Prof.Sigala.
Mashabiki wa Diamond wamepokea kwa
furaha taarifa hizi na wengine wameanza
kurusha vijembe mitandaoni kujibu
mapigo ya waliomzomea Diamond kwny
tamasha la Fiesta mwaka huu.
Mdau mmoja wa karibu wa Diamond
amenukuliwa kwny ukurasa wake wa
Facebook akisema “Ningependa
kuwakaribisha Wazomeaji woooteee
wenye sauti mbaya sana waweze kufika
kwenye Viwanja vya UDSM kushuhudia
Tukio la Kihistoria kwa Mtoto huyu wa
Tandale ambaye ni BIDII NA HESHIMA
Vimemfikisha hapa.”
Ikiwa “Senate” ya UDSM itapitisha
maombi hayo, na Diamond kutunukiwa
Shahada hiyo basi atatambulika rasmi
kama DR.NASIBU ABDUL au Pengine
DR.DIAMOND PLATNUMZ au ukitaka
swaga unaweza sema DR.PLATNUMZ
BABY!
Baadhi ya watu wameonekana
kutoridhishwa na mapendekezo hayo ya
Idara ya Sanaa ya chuo kikuu cha Dar
kumtunuku Diamond PhD, huku wengine
wakinukuliwa wakisema “Ukistaajabu
Uprofesa wa JK utaona PhD ya Diamond”
SOURCE: JF

Breaking: CHIDI BENZ AFANIKIWA KUPATA DHAMANA


Hatimaye Rapa Chid Benz leo amefanikiwa
kupata dhamana na kutolewa rumande na
kurejea uraiani. Anatakiwa kufika
mahakamani Novemba 11 ambapo kesi yake
itatajwa tena.
Una lipi la kumwambia Chid Benz baada ya
kupata dhamana na kurejea uraiani?

Tuesday, October 28, 2014

Breaking: MHIMBILI WAPANDISHA GHARAMA ZA VITANDA

Kwa mujibu wa taarifa iliyosainiwa na
Mkurugenzi mtendaji wa hospitali hiyo, Dk
Marina Njelekela na kusambazwa kwenye
vyombo vya habari, Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili (MNH), imepandisha gharama ambapo
mgonjwa atakayelazwa atalazimika kulipa
Sh5,000 kwa siku.
Taarifa hiyo ilibainisha kuwa gharama mpya
ambazo zitalipwa kwa wagonjwa wote wa rufaa
zilianza kutumika Oktoba 17, mwaka huu
ambapo taarifa zaidi kutoka hospitalini hapo
zimebainisha kuwa tangu utaratibu huo uanze,
kumekuwa na tofauti kubwa na zamani kwa
sababu wagonjwa ambao hawana uwezo wa
kulipia kiasi hicho, hawalali hospitali hata kama
hali zao zingewataka kulazwa.

Monday, October 27, 2014

BREAKING :CHID BENZI KUFIKISHWA MAHAKAMANI


kufikishwa mahakamani kesho Asubuhi
MONDAY , 27TH OCT , 2014
Msanii wa muziki Chidi Benz anatarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya kesho kujibu mashitaka kutokana na kesi ya kukamatwa na Dawa za Kulevya, tukio lililotokea Ijumaa wiki iliyopita.

Kwa mujibu wa Kamanda Geofrey Nzowa, Mkuu wa Kikosi cha kupambana na dawa za Kulevya nchini, Chidi Benz atafikishwa katika mahakama ya Kisutu ambapo atasomewa mashitaka yake kwa mara ya kwanza.
Chidi alipatikana na dawa za kulevya aina ya Heroine kete zipatazo 14 pamoja na misokoto ya Bangi katika kiwanja cha ndege cha Julius Nyerere akiwa anaelekea Mbeya kwa shughuli za kimuziki.

hemed phd ft gelly wa rhymes the one

Shilole - Namchukua (Official Video)

DOWNLOAD MWANA FA FT ALLY KIBA-KIBOKO

Elly bizzy kuhama offcial video

DOWNLOAD NEW SONG SHUKU-WE NI MZURI

BARUA YA DIAMOND (WCB ) KWA JWTZ

Friday, October 24, 2014

Breaking: CHIDI BENZI AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA


Kuna taarifa zilitoka on millardayo.com leo
jioni kuhusu msanii wa muziki wa kizazi
kipya Chidi Benz kukamatwa na dawa za
kulevya katika uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam
akiwa anaelekea Mbeya kwenye show ya
Instagram Party ambayo inatarajiwa
kufanyika kesho.
millardayo.com iliahidi kuzifatilia hizi taarifa
kwa Polisi ili kupata uthibitisho ambapo
imefahamika ni kweli msanii huyu
amekamatwa leo mchana akiwa katika
sehemu ya kuondokea uwanjani hapo
ambapo baada ya alifanyiwa upekuzi na
kubainika amebeba dawa hizo ambapo ni
kete 14 za dawa za kulevya kwenye mfuko
wa shati lake na misokoto miwili ya bangi.
Kwenye mahojiano na millardayo.com
kamishna msaidizi wa Polisi (ACP) Hamisi
Selemani ambae ni kamanda wa polisi katika
viwanja vya ndege Tanzania amethibitisha
kukamatwa kwa Chidi Benz na kusema
msanii huyu alipohojiwa amekiri kweli kuwa
dawa hizo ni zake.
Amesema ‘Alikuja Airport kwa ajili ya safari
kwenda Mbeya, kete hizo 14 za dawa za
kulevya zilikua zimefungwafungwa na nailoni
na pia amekutwa na vifaa vingine
vinavyohusiana na watu wanaotumia dawa za
kulevya, kuna kigae na kijiko na yeye
mwenyewe anakiri ni vitu vyake huwa
anatumia ila anashangaa ni kwa nini
vimeweza kubaki kwenye mfuko,
tutamfikisha Mahakamani baada ya kuweza
kubaini ni dawa aina gani za kulevya’

    

BASATA KUMVUA TAJI MISS TANZANIA


BASATA Kumvua Taji Miss Tanzania 2014 Kwa
Kudanganya Umri
Sakata la lililojitokeza la mrembo wa Taifa wa
mwaka huu 'Redd's Miss Tanzania 2014', Sitti
Mtemvu kudaiwa kudanganya umri, limeingia
katika sura mpya baada ya Baraza la Sanaa
Tanzania (Basata) kueleza kuwa litamvua taji
hilo endapo itabainika kweli alichakachua umri
wake.
Katibu Mkuu wa Basata, Geoffrey Mwingereza,
aliliambia NIPASHE jana kuwa baraza hilo
linasubiri uchunguzi ukamilike na endapo
watabaini kuna udanganyifu ulifanyika
hawatakuwa na la kufanya zaidi ya kumvua taji.
Wakati Mwingereza akieleza hayo, viongozi wa
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo wanatarajia kukutana leo jijini Dar es
Salaam kwa ajili ya kujadili sakata hilo la Sitti.
Akizungumza na NIPASHE jana, Naibu Waziri wa
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Juma Nkamia, alisema serikali
imesikia taarifa za mkanganyiko kuhusiana na
mrembo huyo hivyo imeamua kuitisha kikao ili
kuanza kulifanyia kazi.
Nkamia alisema kamwe serikali
haiwezi kukaa kimya pale ambapo
jina la nchi linatajwa vibaya.
"Siwezi kukuambia hatua gani
zitachukuliwa, ila kesho (leo)
tutakuwa na kikao, serikali haiwezi
kukaa kimya, kuna vyombo vyake
vinalifanyia kazi," alisema Naibu
Waziri huyo.
Aliongeza kuwa yeye alikuwa nje
ya Dar es Salaam, lakini tayari
kuna maelekezo aliyoyatoa na
yameanza kufanyiwa kazi na
wizara hiyo.
Siku moja baada ya Sitti
kutangazwa mshindi wa taji hilo,
taarifa za mrembo huyo kuhusu umri wake
zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii
zikionyesha kuwa ana miaka 25, hivyo hana sifa
za kushiriki shindano hilo hapa nchini.
Nakala ya hati ya kusafiria ya mrembo huyo
ambayo ilitolewa Februari 15, 2007 na muda
wake wa kumaliza kutumika ukiwa ni Februari
14, 2017 yenye namba AB 202696 inaonesha
Sitti ambaye pia anashikilia taji la Kitongoji cha
Chang'ombe na Kanda ya Temeke, alizaliwa
Mei 31, 1989.Pia taarifa nyingine zinazoone sha
mrembo huyo ana miaka 25 ni zilizokuwa
kwenye Taasisi ya Explore Talent, ikimtaja
kwamba anaishi Dallas, Texas, urefu wake ni
5'8, umbo lake ni la kati, asili yake ni Mwafrika
na rangi ya macho yake ni kahawia.
Juzi, Kamati ya Miss Tanzania iliyoko chini ya
Mratibu wa shindano hilo, Hashim Lundenga,
ilisema kuwa Sitti amezaliwa Mei 31, 1991 katika
wilaya ya Temeke jijini kwa mujibu wa cheti
chake cha kuzaliwa alichokionesha.
Lundenga alionesha cheti cha kuzaliwa cha Sitti
ambacho kimetolewa na Wakala wa Usajili,
Ufilisi na Udhamini (RITA) Septemba 9, mwaka
huu kikiwa na namba 1000580309 na kikimtaja
baba yake ni Abbas Mtemvu Zuberi (Mbunge-
Temeke) wakati mama ni Mariam Nassor Juma
(Diwani- Temeke).
Hata hivyo, Lundenga alisema kuwa kamati
yake inaendelea na uchunguzi kuhusiana na
taarifa hizo na endapo watabaini kuwepo na
udanganyifu watamchukulia hatua mrembo
huyo kwa kushirikiana na Basata.
Pia Lundenga na Sitti, walikanusha taarifa za
mrembo kuwa kuwa na mtoto na kusema
kwamba mwenye uthibitisho wa jambo hilo
anatakiwa aliwasilishe kwa kamati ili hatua
zichukuliwe.
Sitti aliibuka kidedea katika shindano la urembo
la taifa lililofanyika usiku wa Jumamosi ya
Oktoba 11 kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini
na kuwashinda washiriki wenzake 29 waliokuwa
wanawania taji hilo.

Sunday, October 19, 2014

MSIKILIZE MENEJA WA T.I AKIONGEA JINSI YA KUFANYA COLLABO NA T.I


Records, Jason Geter amesema ili msanii wa Afrika aweze kupata collabo na msanii mkubwa wa Marekani, anahitajika kuwa na ushawishi katika sehemu anayokotoka ili awe na kitu cha kumuongezea pia msanii huyo anayetaka kumshirikisha. Meneja wa T.I, Joson Gete akizungumza na wadau wa muziki Dar Jason Geter Akiongea kwenye warsha iliyoandaliwa maalumu kwaajili ya wadau wa muziki nchini Ijumaa hii, Geter alitolea mfano wa jinsi T.I. alivyokubali kufanya wimbo na P-Square. Alisema alipigiwa simu na rafiki yake aliyemueleza kuwa kundi la P-Square lingetaka kumshirikisha T.I. kwenye wimbo wake lakini bahati mbaya hakuwahi kuwasikia wasanii hao. “Kiukweli nilikuwa sijawahi kuwasikia kabla, kwasababu Marekani hawachezwi kivile, nina uhakika baadhi ya watu wanawafahamu lakini watu wengi Marekani hawawafahamu kabisa P-Square,” alisema. Geter alidai baada ya kuambiwa hivyo aliamua kufanya utafiti wake mwenyewe ili kuwafahamu wasanii hao na hivyo aliingia Youtube kuwatazama. “Nilipoenda kufanya utafiti wangu, nikasema wow, hawa jamaa ni wakubwa,” aliongeza. Alidai baada ya kuona ukubwa wake, aliona kuwa P-Square wana kitu cha kumuongeza T.I. “Sababu mashabiki wengi wa P-Square wanaweza kuwa hawajawahi hata kumsikia T.I. Kwahiyo hicho ndio kitu cha kwanza kwamba utaenda kumuongezea nini msanii wangu. Msanii wangu ana msingi wa Marekani kukupa, wewe utaweza kumtambulisha kwa kitu kingine?” Aliongeza kuwa hatua ya pili inahusisha masuala ya fedha na biashara ambapo huusikiliza wimbo anaotaka kushirikishwa msanii huyo. Alisisitiza kuwa mara nyingi suala la fedha au malipo ya collabo sio kitu wanachokiweka mbele zaidi ya kuzingatia kuwa ni nini msanii wake atakipata kutokana na kushirikishwa kwenye wimbo huo. “Sawa unayo fedha, sasa hatua ya pili, kitu gani unaweza kukioffer kwake, una kitu cha kuoffer kwa msanii wangu? Je wimbo ni mzuri? Kwahiyo hivyo ndio vitu ambavyo unahitaji kuvifikiria. Na mwisho wa siku zote unatakiwa kulinda brand yako.” Kuhusu njia anayotakiwa msanii kufanikiwa katika soko la muziki wa Marekani, Jason alisema jambo la kwanza ni kuwa na ukaribu na watu kama yeye ambao wana connection na watu wengi pamoja na brands ambazo zimesimama nchini humo. Geter alidai kufanya wimbo na msanii wa Marekani peke yake, haitoshi kwa msanii wa Afrika kufanikiwa kwenye soko la Marekani. “T.I. alifanya ngoma na P-Square, lakini kiukweli, inahitaji zaidi ya hivyo kupenya soko la Marekani,” alisisitiza Geter. “Inahitaji T.I. na P-Square kwenda kwenye game ya basketball pamoja na kutembea pamoja. Inahitaji uwekezaji huo wa muda kwa msanii wa Afrika kutumia muda kukaa kwenye soko la Marekani.” Geter alisisitiza kuwa kama msanii anataka kufanikiwa Marekani, anatakiwa kutake risk kwa kuacha fedha nyingi anazopata Afrika na kukubali kupata kidogo Marekani wakati anakuza jina lake. “Kama unaingiza dola 5 Afrika, unaweza kuja Marekani na utakuwa na bahati sana ukipata sehemu sahihi ambazo unaweza ukapata hata dola moja tu. Ni kazi sana kwa watu kuwekeza muda wa aina hiyo na nguvu katika chochote kile, hiyo ndio changamoto kubwa.” Geter alisema hilo linawezekana kwa kuingia ubia na watu ambao tayari wana nguvu huko kukusaidia. Kuhusu lugha ambayo msanii anatakiwa kutumia, Geter alisema muhimu ni kufahamu kuongea Kiingereza lakini sio lazima nyimbo ziwe za lugha hiyo kwakuwa muziki unaweza kufanya vizuri hata kama ukiwa umeimbwa kwa lugha nyingine. “Lakini yote ni kuwa kile ambacho tunafanana ni rhythm. Ni ile beat inayonifanya nicheze na pia hisia ambayo inagusa moyo. So in America to get played on radio and all that stuff, yes you need to know some English but if you got that beat right, we gonna move man.”msikilize apa

Thursday, October 16, 2014

KIJANA APIGISHWA MBIZI KWENYE DIMBWI

Askari wa jeshi la Wananchi
la Tanzania (JWTZ)
akimwadhibu kijana ambaye
hakuweza kufahamika jina lake
mara moja, kwa kumpigisha
mbizi kwenye dimbwi la maji
ya barabarani baada ya
kukutwa akiwa ametinga sare
za Jeshi la Wananchi huku
akipiga misele mitaani
wakati akitambua kuwa yeye
si askari ni raia wa
kawaida.
Kijana huyo alikutana na
adhabu hiyo kali kutoka kwa
mjeda huyo baada ya kumbaini
kuwa si askari halisi ya
jeshi la Tanzania wakati
alipokamatwa na kushindwa
kutoa maelezo ya kuridhisha
kuhusiana na swala zima la
kijeshi, na hapo ndipo
alipoanza kuamuliwa kuvua
mavazi hayo na kisha kuaza
kutumikia adhabu hiyo.
Tukio hilo lilitokea hivi
karibuni maeneo ya Kariakoo
jijini Dar es Salaam.
Kijana akiendelea kutumikia
adhabu ya kupiga mbizi.
Picha na Kamanda wa Matukio
Blog.Mia

DOWNLOAD WIMBO HUU WA ZACHAA FT DIAMOND

DOWNLOAD WIMBO WA MICHA PELO NILIAMUA MP3

DOWNLOAD WIMBO WA MICHA PELO FT ALLY NIPISHE MP3

DOWNLOAD WIMBO WA ELLY BIZZ mp3

DOWNLOAD WIMBO WA MASE H-MONEY MP3

Wednesday, October 15, 2014

HALIMA JAMES MDEE AFUNGUKA MAZITO



MBUNGE wa Jimbo la Kawe jijini Dar na
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha),
Halima James Mdee ambaye aliwekwa
Mahabusu ya Gereza la Segerea, Dar kwa saa
kumi na mbili amesimulia mambo matano
mazito aliyokumbana nayo hali iliyomfanya
atokwe machozi.
Mbunge wa Jimbo la Kawe jijini Dar
na Mwenyekiti wa Baraza la
Wanawake wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo
(Bawacha), Halima James Mdee.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii
mwishomi mwa wiki iliyopita, Mdee licha ya
kuponda utendaji kazi mbovu wa serikali
kuhusu mahabusu, aliyataja mambo hayo kama
ifuatavyo:
HAUSIGELI NA KESI NDOGONDOGO
Alisema alipofika mahabusu aliwakuta
wasichana wadogo ambao baadhi yao ni
mahausigeli wakamlalamikia kwamba wamekaa
ndani kwa muda mrefu bila kesi zao kusikilizwa.
Alisema kwa uchunguzi wake alibaini kuwa
wasichana hao wa kazi za ndani, kesi zao
zilifunguliwa kwa kubambikwa na mabosi wao
pale wanapodai malipo, hivyo wao husingiziwa
wizi au kosa lolote.
UBOVU WA CHAKULA
Pia Mdee alisema chakula cha mahabusu
hakiridhishi kutokana na kupikwa bila kiwango
na kuwa na michanga, wakati mwingine hakiivi.
MAHABUSU KUKAA MUDA MREFU
BILA KESI KUSIKILIZWA
Jambo jingine alilodai kukumbana nalo Segerea
ni mahabusu kukaa kwa muda mrefu kati ya
miaka 4 hadi 7 bila kesi zao kusikilizwa kwa
kisingizio cha upelelezi kutokamilika.
MACHANGUDOA KUWASHAWISHI
MABINTI
Katika sakata lingine, Mdee alisema wanawake
wengi waliokamatwa kwa makosa ya kujiuza
usiku (machangu) wanaopelekwa mahabusu
wamekuwa wakiwashawishi wasichana wadogo,
hasa mahausigeli wanaofikishwa humo.
“Wasichana hao huwashawishi mahausigeli kiasi
kwamba wanapotoka mle mahabusu na wao
wanakwenda kujihusisha na ukahaba na
biashara ya madawa ya kulevya kwa vile baada
ya kutoka hawapewi nafasi na mabosi wao
kuendelea na kazi,” alisema Mdee.
MAHABUSU WA KIKE KUADHIBIWA
NA ASKARI WA KIUME
Jambo lingine aliloligundua Mheshimiwa Mdee
ni kitendo cha askari wa kiume kutoa adhabu
kwa maabusu wa kike badala ya kuadhibiwa na
wanawake wenzao kitendo ambacho alisema
kimekuwa kikiwadhalilisha mahabusu hao.
Hata hinyo, Mdee alimuomba Waziri wa Sheria
na Katiba, Asharose Migiro kuanzisha utaratibu
wa safari za kushtukiza magerezani na
kuzungumza na mahabusu ili kusikiliza kero zao
na kuzitatua.
Jumanne iliyopita, Mdee alifikishwa katika
gereza hilo saa 11 jioni ambako alilala hadi
kesho yake saa 1 asubuhi kwa madai ya
kufanya maandamano haramu kwenda Ikulu ya
Dar.